Monday, February 3, 2014

Enzi hizo

Mapumziko wakati wa shooting ya Bwana ni nuru yangu eneo la chamazi Dar es salaam.
Wawa ni baadhi wa waanzilishi wa kwaya ya vijana kijitonyama. Picha hii ilipigwa katika usharika wa kijitonyama mwaka 1999. Eneo hili kwa sasa kuna jengo la kitega uchumi cha usharika.

Ijue Kwaya ya Vijana Kijitonyama

KWAYA YA VIJANA KIJITONYAMA LUTHERAN
UTANGULIZI
Ni kikundi kilichoundwa kwa madhumuni ya kueneza injili kwa njia ya uimbaji. Msukumo wa kuunda kikundi ulitokana na msukumo uliokuwa ndani ya waanzilishi baada ya kuona nguvu ya uimbaji katika kuvuta wengi na kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao.
MADHUMUNI
  • Kutangaza Neno la Mungu kwa njia ya uimbaji
  • Kuwasaidia watu wakue katika maadili mema kwa njia ya Neno la Mungu, maombi na ushirika
  • Kujenga mahusiano mazuri miongoni watu wote
  • Kushiriki katika maendeleo ya kijamii
  • Kuinua na kuendeleza muziki wa injili
  • Kutoa huduma ya uimbaji vyuoni na mashuleni
  • Kutoa huduma kwa wajane, yatima na wasiojiweza
MAFANIKIO
Kwaya ya Vijana ambayo ilianzishwa zaidi miaka 10 iliyopita imeshiriki na kutoa huduma ya uimbaji sehemu zifuatazo:-
  • Makanisani
  • Mikutano ya injili
  • Kumbukumbu za Martin Luther Jr. katika Ubalozi wa Marekani
  • Ufunguzi wa ofisi mpya za Ubalozi wa Marekani
  • Kumbukumbu ya uhuru wa marekani
  • Kumbukumbu ya kulipuliwa ofisi za Ubalozi wa Marekani
  • Matamasha ya uimbaji katika mikoa mbalimbali ya Tanzania
  • Kwenye misiba kuwafariji Wafiwa
  • Kwenye maharusi na sherehe mbalimbali za kumtukuza Mungu
  • Katika utumishi wetu watu wengi wamebadilisha maisha yao na kupokea wokovu wa Mungu baada ya kusikia nyimbo zetu, na baadhi yao wamekuja kutushudia.
  • Kwenye makongamano ya vyuo na shule za sekondari
  • Mbali kufanya huduma za kiroho Kwaya pia imesaidia maendeleo ya kijamii kama ifuatavyo:-
  1.     Huduma za Yatima na Wajane
  2.    Imewasaidia baadhi ya vijana ambao hawakuwa na msaada wa kupata elimu kwa kuwalipia ada na wengi wamepata ajira nzuri baada ya kumaliza masomo yao
  3.     Kuwatafutia ajira vijana wasiokuwa na ajira ndani na nje ya kwaya
MATATIZO
  • Uchakavu na upungufu wa vyombo vya muziki umerudisha nyuma maendeleo ya huduma yetu kwa kiasi kikubwa.
  • Kuna changamoto ya ajira kwa vijana wanaojiunga na kwaya mara kwa mara
OMBI
Ili kuiwezesha huduma hii nzuri isirudi nyuma bali isonge mbele kwanza tunahitaji maombi yako na pia msaada wa hali na mali.

Ijue kwaya ya vijana kijitonyama

KWAYA YA VIJANA KIJITONYAMA

MFUMO WA UIMBAJI KATIKA KWAYA YETU

Kama yalivyoandaliwa na:
Mwalimu wa kwaya; Gadiel Ketto.
October 16, 2002
Yafuatayo ni mapendekezo ya taratibu za uimbaji katika kwaya ya vijana. Msukumo wa
mapendekezo haya ni kuweka mfumo mzuri na madhubuti usio badilikabadilika kulingana na mabadiliko yoyote yayoweza kutokea katika kwaya. Mabadiliko yaweza kusababiswa na kubadilika kwa waimbaji, waalimu, au viongozi. Pia misukumo toka nje ya kwaya yaweza pia kuleta mabadiliko. Hivyo ili tuweze kuwa na mfumo imara wa uimbaji, tunapendekeza yafuatayo:-

1. AINA YA UIMBAJI
Aina ya uimbaji ni ile inayombariki Mungu na wanadamu. Lakini wanadamu huwa wana
vionjo vingi na vinavyotofautiana. Hivyo ili tuweze kumgusa kila mtu yafaa sisi kama
waimbaji au wasanii tuweze kuangalia kuwa hadhira inataka nini kwa ujumala bila kuangalia na kuridhisha sehemu tu ya kundi la watu. Faida yake ni kuwa ujumbe wetu katika nyimbo utaweza kuyagusa makundi yote katika jamii na kufanikisha malengo yetu. Kwa hiyo basi tuwe na uimbaji wa aina mbalimbali kama vile pambio, nyimbo za haraka haraka, nyimbo za taratibu na nyimbo za kawaida zilizozoeleka katika muziki wa kanisani.

2. NYIMBO
Kama kwaya tunapaswa kujifunza na kuimba nyimbo mbalimbali. Ni vyema nyimbo zetu
zikawa katika makundi yafuatayo:-
a).Nyimbo za zamani (classic music)
Hizi ni nyimbo zilizoandikwa zamani ambazo zina "melody" nzuri na ujumbe mzuri.
Hizi zifundishwe na.kuimbwa katika kwaya yetu.
b).Nyimbo za kutunga / kuandika wenyewe (contemporary music).
Nyimbo hizi ni nzuri zaidi, zinachochea ubunifu na vipaji tulivyonavyo. Ni vizuri tukaandika na kuimba nyimbo kulingana na jamii ya sasa na kwa faida ya vizazi vijavyo. Tukumbuke kuwa hata nyimbo za zamani tunazoimba leo ziliandikwa na watu kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Kama babu zetu wasingeandika tusingekuwa na nyimbo nzuri za kuimba kama tunavyofahamu. Kwa hiyo tujue kuwa kama hatutaandka nyimbo leo, watoto wetu hawatakuwa na kitu cha kujivunia ambacho tumewarithisha kwa ajili ya Bwana. Pia tukwepe kuimba nyimbo za watu wengine, walioandika wenyewe na kuimbwa na watu wengine kwa kuzingatia sheria ya haki-miliki tukijua kuwa hata tukiimba hatuwezi kuzirekodi.

3. MUZIKI / ALA (ACCOMPANIMENT)
Ni vizuri kumwimbia Mungu kwa kutumia vyombo mbalimbali ambavyo vinasaidia
kuusindikiza ujumbe. Vyombo hivyo ni kama gitaa, keyboard, tarumbeta, ngoma, nk.
Inafaa kuwa na utaratibu mzuri wa kuvitumia bila kuleta fujo na kelele katika uimbaji. Hili tu litawezekana endapo tutatafuta na kuwaandaa wanamuziki wetu katika kwaya hii.

4. UFUNDISHAJI WA NYIMBO
Kwaya nzuri ni ile yenye waalimu wengi angalau watano wenye vipaji na utaalamu katika fani ya muziki. Hawa lazima wawe na sauti moja ili kifanya kwaya iwe moja uimbaji mmoja na usiobadilika. Kiburi na kujikweza iwe mwiko kwa walimu wa kwaya hii. Pia kuwe na utaratibu mzuri wa kufundisha nyimbo kwa kupeana nafasi na kushirikiana katika kuboresha. Kwa upande huu pia ni vyema wale wenye vipaji wakatiwa moyo ili kusomea fani ya muziki.

5. UBORESHAJI WA UIMBAJI
Kama waswahili wasemavyo ukiamua kumla nguruwe chagua aliyenona, vivyohivyo na
sisi kama tumenamua kuimba ni vyema tukaimba vizuri. Hivyo ni vizuri tukazingatia mazoezi ya mara kwa mara ya uimbaji na kuhakikisha kuwa kila mwanakwaya anashiriki. Mazoezi haya yafanyike kila siku za mazoezi, kuandaa kambi, na hata kufanya mikesha maaalumu ya mazoezi ya uimbaji.

Friday, January 31, 2014



Monday, March 19, 2012

Mungu ni mwema

Karibuni wote